Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nigeria yahamisha mechi ya Libya

19391 Pic+nigeria TanzaniaWeb

Thu, 27 Sep 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Abuja, Nigeria. Shirikisho la soka la Nigeria (NFF), limeamua kuuhamisha mchezo wa kufuzu fainali za Afrika 2019, kutoka uwanja wa Ahmadu Bello mjini Kaduna na kuupeleka mjini Uyo kwa tarehe ileile.

Uamuzi huo umetokana na uwanja huo wa Ahmadu Bello kukosa vigezo baada ya ukaguzi wa kawaida uliofanywa na shirikisho la soka la Afrika (Caf), kuvikagua viwanja mbali mbali barani humo.

Katika taarifa ya NFF, mchezo huo wa kufuzu kwa fainali za Afrika sasa utafanyika kwenye uwanja wa Godswill Akpabio mjini Uyo, baada ya Caf kuukataa uwanja wa Ahmadu Bello, kutokana na pichi yake kuharibika na kuwa hatari kwa wachezaji.

“Nyasi za uwanja wa Ahmadu Bello hazipo kwenye ubora wake na Caf  wameukataa kwa hiyo inatulazimu kuuhamisha mchezo dhidi ya Libya,” ilisema taarifa ya NFF.

Kocha wa Super Eagles, Gernot Rohr, raia wa Ujerumani, alisema uamuzi huo hautaathiri kwa namna yoyote maandalizi ya timu yake kuelekea mchezo huo utakaopigwa mwezi ujao.

Chanzo: mwananchi.co.tz