Beki wa zamani wa Manchester United, Gary Neville amewatuhumu wachezaji wa klabu hiyo kwa kutoipambania timu na kufanya mambo kama watoto huku wakidhani wao ni bora kuliko ilivyokuwa enzi zao, wakati wanakubali kipigo cha bao 4-2 dhidi ya Leicester City Jumamosi.
Pia Neville amemsisitizia kocha Ole Gunnar Solskjaer kufanyia kazi madhaifu ya kikosi chake ikiwa ni pamoja na kuifanya timu kuwa na mshikamano ili kuondokana na mwenedo mbaya wa matokeo wanayoyapata uwanjani
Beki huyo wa zamani wa "Mashetani Wekundu" anasema kuwa haya sio matokeo ya kwanza ya kukatisha tamaa yaliyopatikana na timu ya Ole Gunnar Solskjaer kwani mpaka sasa tayari wamepoteza kwa Young Boys, Aston Villa na West Ham msimu huu.