Thu, 22 Mar 2018
Chanzo: bongo5.com
Mchezaji tennis raia wa Japani, Naomi Osaka amefanikiwa kuendelea na michuano ya wazi ya Miami (Miami Open) baada ya kumtoa Mmarekani, Serena Williams katika mzunguko wa kwanza.
Osaka ameonekana kuzidi kufanya vizuri katika mchezo wa tennis na kupanda hadi nafasi ya 22 kwenye viwango vya mchezo huo duniani baada ya kutwaa ubingwa wa WTA Indian Wells amemtoa Mmarekani huyo kwa seti 6-3 6-2.
Williams ambaye amerejea WTA Tour Californian mapema mwezi huu baada ya kupita miezi 14 toka kujifungua mtoto wake wa kwanza.
Chanzo: bongo5.com