Mwanariadha wa Ethiopia Tigist Assefa Jana Jumapili amevunja rekodi ya Wanawake kwenye Berlin Marathon na vilevile kushinda katika mbio hizo.
Assefa (29) ambaye pia alishinda mwaka jana, aliuvuka mstari wa ushindi baada ya kutumia masaa 2 dakika 11 na sekunde 53, 2:11.53
Mwanariadha huyo ambaye alianza mashindano ya Marathon mwaka jana amevunja rekodi iliyowekwa na Mwanariadha wa Kenya Brigid Kosgei mwaka 2019 ya 2:14.04
Kabla ya kuingia kwenye Marathon Assefa alikuwa mtaalamu wa mita 800.
Bingwa mara mbili wa Olimpiki Eliud Kipchoge (38) ameongoza kwa upande wa wanaume kwa mara ya tano huko Berlin kwa muda wa 2:02.42