Mon, 28 Oct 2019
Chanzo: mwananchi.co.tz
Mwanariadha Private Alphonce Simbu amefanikiwa kupeperusha bendera ya Tanzania katika Mashindano ya Majeshi ya Dunia na kujinyakulia Medali ya Fedha ( Silver).
Mwanariadha huyo kutoka Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania alimaliza mbio hizo ndefu za Kilometa 42 baada kukimbia kwa muda wa 2: 11.16 na kuwashinda wengie zaidi ya 90 kutoka zaidi ya nchi 30.
Mshindi wa Kwanza ni Luche Sumi kutoja Bahrain aliyekimbia 2:08.28
Mshindi wa Tatu ni mwanariadha kutoka Rwanda John Hakizimana akiyekimbia kwa karibu nyuma ya Simbu kwa 2:11:19.
Chanzo: mwananchi.co.tz