Sun, 1 Apr 2018
Chanzo: bongo5.com
Mshambuliaji wa klabu ya Liverpool ya nchini Uingereza, Mohamed Salah hii leo ameisadia timu yake kuchomoza na ushindi wa jumla ya mabao 2 – 1 dhidi ya Crystal Palace na kuifanya kushika nafasi ya pili kwa muda kwenye msimamo huo kabla ya Manchester United haijakutana na Swansea hapo baadae.
Salah amefunga bao la pili dakika ya 84 lililosaidia kuchomoza na ushindi huo unao ifanya Liverpool kufikisha jumla ya pointi 66 dhidi ya 65 za Man United huku mshambuliaji huyo hatari raia wa Misri akifikisha jumla ya mabao 37 kwenye mashindano yake yote msimu huu.
Chanzo: bongo5.com