Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Michezo ya Olimpiki ya Paris yafika tamati

Michezo Ya Olimpiki Ya Paris Yafika Tamati.png Michezo ya Olimpiki ya Paris yafika tamati

Mon, 12 Aug 2024 Chanzo: Bbc

Nyota wa michezo na muziki walikusanyika pamoja katika sherehe za Paris 2024 ili kukamilisha mashindano ya Michezo ya 33 ya Olimpiki.

Mwigizaji Tom Cruise alikuwa katika uwanja wa Stade de France na kuchukua bendera ya Olimpiki kama sehemu ya makabidhiano kwa jiji la Marekani la Los Angeles, ambalo litakuwa mwenyeji wa Michezo inayofuata mnamo mwaka 2028.

Red Hot Chili Peppers, Billie Eilish, Snoop Dogg na Dr. Dre kisha wakatumbuiza kwenye Ufuo wa Venice kama sehemu ya kuhitimisha sherehe hiyo.

Hapo awali, ndani ya uwanja wa michezo wa Paris, washindi wa medali za dhahabu Alex Yee na Bryony Page walikuwa washika bendera wa Uingereza kwenye sherehe hiyo.

Uingereza ilimaliza katika nafasi ya saba kwenye jedwali la medali ikiwa na dhahabu 14, fedha 22 na shaba 29. Ikiwa ni jumla ya idadi ya medali 65, moja zaidi ya 64 walizoshinda Tokyo 2020.

Katika hotuba yake ya mwisho, rais wa Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki (IOC) Thomas Bach alizungumzia Michezo hiyo "ya kuvutia".

Michezo ya Olimpiki ya Walemavu ya 2024 itafanyika katika mji mkuu wa Ufaransa kutoka 28 Agosti hadi 8 Septemba.

Chanzo: Bbc