Tue, 13 Mar 2018
Chanzo: bongo5.com
Kiungo wa Manchester United, Michael Carrick ametangaza rasmi kustaafu soka mwishoni mwa msimu huu.
Carrick mwenye umri wa miaka 36, amecheza jumla ya michezo 463 ndani ya United toka ajiunge akitokea Tottenham kwa pauni milioni 18 mwaka 2006 na kufanikiwa kushinda mataji 34 nchini Uingereza.
Kiungo huyo amesema kuwa unafika muda mwili wako unakuambia ‘stop’, na hivyo ndivyo ilivyo kwangu kwa sasa.
Mwezi Januari meneja wa timu hiyo, Jose Mourinho amesikika akisema kuwa angelijiskia furaha endapo Carrick ataamua kusalia ndani ya klabu
Chanzo: bongo5.com