Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Meneja Wa Metacha Afunguka Kusajiliwa Simba - Video

Video Archive
Tue, 29 Jun 2021 Chanzo: globalpublishers.co.tz

Meneja Wa Metacha Afunguka Kusajiliwa Simba – Video June 29, 2021 by Global Publishers

METACHA Mnata, anaweza kwenda Azam FC ama Simba ikiwa mabosi wake wa sasa Yanga watakaa kimya juu ya mkataba wake.

Nyota huyo ambaye amesimamishwa na Yanga kwa muda usiojulikana huku akikutana na rungu kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, (TFF) kutocheza mechi tatu pamoja na faini ya laki tano dili lake linameguka msimu huu.

Kosa lake ilikuwa ni kuwaonyesha ishara ya matusi mashabiki wa Yanga katika mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Ruvu Shooting, Uwanja wa Mkapa ambapo Yanga ilishinda kwa mabao 3-2.

Kwa mujibu wa Meneja wa Mnata, Jemedari Said amesema kuwa yupo tayari kupokea ofa kutoka Azam FC na Simba endapo Klabu ya Yanga itakaa kimya. ⚫️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP: ⚫️ ANDROID:http://bit.ly/38Lluc8 ⚫️ iOS:https://apple.co/38HjiCx

Chanzo: globalpublishers.co.tz