Thu, 25 Jan 2018
Chanzo: bongo5.com
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limesogeza mbele kwa siku moja mchezo namba 114 kati ya Mwadui FC ya Shinyanga na Njombe Mji ya Njombe uliokuwa ufanyike Ijumaa Januari 26, 2018 kupisha mazishi ya aliyekuwa kocha msaidizi wa Mwadui Jumanne Ntambi.
Aliyekuwa kocha msaidizi wa Mwadui FC, Jumanne Ntambi
Mchezo huo sasa utachezwa Jumamosi, Januari 27, 2018.
Kocha huyo msaidizi wa Mwadui alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu kabla ya kufikwa na mauti
Chanzo: bongo5.com