Tue, 14 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchezaji wa zamani wa American football DJ Hayden (33), amefariki dunia katika ajali mbaya ya gari iliyotokea Jumamosi huko Houston, Texas nchini Marekani.
Hayden alikuwa kati ya watu sita waliopoteza maisha katika ajali hiyo iliyotokea baada ya gari aina ya Chrysler 300 kuendesha kwa kasi, kuzipita alama za taa nyekundu hadi ugongana na SUV.
Hayden, Mchezaji wa zamani wa NFL amewahi kuchezea timu za Oakland Raiders, Detroit Lions na Jackson Ville Jaguars katika miaka ya 2013 hadi 2020.
Mwaka 2021 alikuwa sehemu ya timu ya Washington Commanders.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live