Zanzibar inaweza kuingia kwenye historia ya mchezo wa magari na kuifanya Tanzania kuwa taifa la pili barani Afrika baada ya Afrika Kusini kupata haki ya kuandaa mashindano ya mbio za magari ya Formula 1 maarufu kama Langalanga.
Kwa mujibu wa Jarida la la Michezo la nchini Italia - Sportface, Zanzibar imetuma maombi ya kuandaa michuano hiyo mikubwa duniani ambapo inachuana na taifa la Afrika Kusini lenye faida zaidi kutokana na maeneo yake Kijiographia.
Zanzibar wanaripotiwa kuwa wamekuwa wakituma maombi hayo kwa kipindi cha miaka mitano sasa kuomba uenyeji kwenye michuano yoyote kulingana na Kalenda ya Formula 1, na sasa ombi hilo limeanza kuzingatiwa.