Thu, 2 Aug 2018
Chanzo: mwananchi.co.tz
Kartepe. Kocha Mkuu wa Simba, Mbelgiji Patrick Ausemms amesema, anauchukulia mchezo wa kesho Jumatano na Mouloudia ya Morocco kama sehemu ya mazoezi yake.
Mbelgiji huyo ambaye katika mazoezi ya sasa ameanza kusaka kikosi chake cha kwanza.
Amesema, ameamua kicheza mchezo huo ambao ni mmoja kati ya mitatu waliyojipangia kuona anapata kikosi anachokihitaji.
"Mchezo huo kwangu nauchukulia kama sehemu ya mazoezi katika kutengeneza timu,"alisema Ausemms
Simba inaendelea na maandalizi yake katika mji wa Kartepe nchini Uturuki.
Chanzo: mwananchi.co.tz