MZIMU wa Green Warriors, umeendelea kuitafuna Simba kwa kuondolewa tena kwenye kombe la FA na Mashujaa FC ya daraja la kwanza kwa kufungwa mabao 3-2.
Simba wametolewa kwenye mashindano ya Kombe la Shirikisho baada ya kufungwa mabao 3-2 na Mashujaa ya Kigoma inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza, katika Uwanja wa Taifa Simba waliingia kwenye mchezo wa leo wakiwa na kumbukumbu ya kuondolewa msimu uliopita kwenye hatua kama hii na Green Warriors kwa changamoto za mikwaju ya penalti. Anayeweza kubebeshwa lawama kwenye mchezo wa leo ni mlinda malango wa Simba, Deogratius Munish 'Dida' ambaye amefungwa kwa shuti dhaifu la Rajabu Athuman lililompita mikononi.