Mwanasoka ghali duniani kwa sasa wa klabu ya PSG, Neymar Jr, amejiwa juu na mashabiki baada ya kupost picha na kujifananisha na mwanasayansi nguli na mnajimu, Stephen Hawking aliyefariki Jumatano hii akiwa na umri wa miaka 76.
Kupitia mtandao wa Instagram Neymar ameweka picha akiwa kwenye kiti cha wagonjwa chenye magurudumu (Wheel Chair) na kuandika ujumbe unaosomeka, “Unapaswa kuwa na mtazamo mzuri na kupata bora zaidi ya hali uliyo nayo. Stephen Hawking. Stephen Hawking.”
Hapa chini ni baadhi ya comment za mashabiki kwenye picha hiyo.
Nooruddean: Neymar there, with his sore metatarsal and sprained ankle, marking Stephen Hawking’s death by cheerily comparing himself to quadriplegic Stephen Hawking