Mashabiki wawili wa Simba kutoka Nyasaka wilayani Ilemela Mkoa wa Mwanza wamefika uwanja wa CCM Kirumba kuushuhudia mchezo wa timu yao dhidi ya Ruvu Shooting wakiwa wamebeba maua.
Wamesema maua hayo ni kwa ajili ya kumkabidhi Msemaji wa Ruvu Shooting, Masau Bwire kwa kile walichoeleza kuwa ni kumpa pole kwa kipigo kizito atakachopokea leo jioni cha mabao 3-0.
Wamesema kutokana na kauli zake za kuichukulia poa timu yao ya Simba wameamua kuja na maua hayo ili yamfariji kwa atakachokutana nacho baadae.
Mashabiki wanaendelea kumiminika uwanjani uwanjani hapo ili kuzishuhudia timu hizo zikimenyana baadae saa 10 jioni.