Meneja wa klabu ya West Ham United, Manuel Pellegrini amelishukuru jeshi la polisi la nchini Chile baada ya kunusurika mikononi mwa vibaka wenye silaha kali wakati walipotaka kupora.
Kupitia mtandao wake wa kijamii wa Twitter, Pellegrini amewashukuru polisi wa nchi hiyo kwakufika muda muafaka eneo la tukio mara baada ya vibaka hao waliyokuwa na silaha za moto walipo wavamia wakati kocha huyo akiwa na mkewe, Carola Pucci kwenye ‘restaurant’ huko Santiago suburb Vitacura usiku wa Jumamosi.
Ujumbe huo unasema kuwa ”Pongezi kwa @Carabdechile kwa kufika haraka na kwa ujasiri. Naheshimu mchango mkubwa wawatu. Natumaini pewa nguvu kubwa na jeshi la polisi katika kutatua matatizo ya kiuhalifu haraka zaidi pale linapo tokea.
Felicitaciones a @Carabdechile por su rápida y valiente reacción. Agradezco el apoyo de la gente. Ojalá se le otorguen mas facultades a Carabineros para solucionar el tema de la delincuencia lo antes posible.
— Manuel Pellegrini R. (@Ing_Pellegrini) June 3, 2018