Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Manchester City kuanza usajili wake wa kwanza kwa kiungo wa Napoli ya Italia

9694 Jorginho Cropped Cqsrpd6vqihu1rwrucymr9449 TZWeb

Thu, 21 Jun 2018 Chanzo: bongo5.com

Mabingwa wa ligi kuu nchini Uingereza Manchester City wanatarajia kukamilisha usajili wake wa kwanza msimu huu kwa kuingia mkataba na kiungo wa kati wa klabu ya Napoli ya nchini Itali, Jorge Luiz Frello Filho maarufu kama Jorginho kwa dau la pauni milioni 46.5.



City ambayo haijaingia kandarasi na mchezaji yeyote toka dirisha la usajili kufunguliwa inatarajia kumsaini, Jorginho mwenye uraia wa nchi mbili Brazil na Italia mwishoni mwa wiki hii.

Napoli wanatarajia kutangaza mbadala wa Jorginho mara baada ya mchezaji huyo kuhamia City rasmi  dili ambalo linatarajiwa kukamilika wikiendi hii.

City pia inahitaji kumsajili Riyad Mahrez kutoka kwenye klabu ya Leicester lakini bado ipo kwenye mazungumzo na timu hiyo juu ya dau la pauni milioni 65 linalo hitajika kwa kiungo huyo mshambuliaji.

Loading...
Chanzo: bongo5.com