Fri, 11 May 2018
Chanzo: bongo5.com
Mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano ndani ya klabu ya Simba, Haji Manara amemwagia sifa kiungo wake raia wa Rwanda, Haruna Niyonzima kuwa ni mchezaji pekee aliyepata bahati ya kutwaa taji la ligi kuu Tanzania Bara mara nne mfululizo kuliko yeyote.
Manara kupitia ukurasa wake wa kijamii wa Instagram ameandika kuwa Niyonzima anakuwa mchezaji wa kwanza kushinda ubingwa wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara mara nyingi tena kwa mfululizo.
Haruna Niyonzima anakuwa mwanadaamu wa kwanza duniani kushinda ubingwa wa Tanzania mara nne mfululizo kwa vilabu viwili tofauti…rekodi hii haijawekwa na yoyote bongo.
Loading...
Chanzo: bongo5.com