Dar es Salaam. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, amenunua jezi ya timu ya taifa 'Taifa Stars' kwa bei ya Sh 5 milioni.
Kiasi hicho cha fedha ni zaidi ya mara 16 ya gharama halisi ya jezi hiyo ambayo inauzwa kuanzia Sh30,000.
Mama Samia amenunua jezi hiyo ni mchango wake katika harambee ya kuichangia timu ya taifa 'Taifa Stars' inayoshiriki Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) huko Misri kuanzia Juni 21 hadi Julai 19.
Makamu wa Rais alisema kuichangia timu ya taifa ni jambo la fahari na hivyo yeye kama kiongozi ni lazima aonyeshe mfano kwa vitendo.
"Tulianzisha kampeni ya kuichangia timu ya taifa ya wanawake lakini kwa bahati mbaya mechi ya kwanza tu ikapoteza.
“Leo nimekuja hapa na Mjukuu wangu Mai ambaye amevaa jezi za timu ya taifa na amesema atachanga kiasi cha Sh 5,000 ila ameniambia anataka nami nimnunulie jezi ya timu ya taifa.”
Pia Soma
- Mabilioni kujenga barabara Dar- Morogoro hadi Dodoma
- Donald Trump achangiwa Sh55 bilioni za kampeni ndani ya saa 24
- Mbunge ataja aina pekee ya gari inayofika jimboni kwake
- Sababu ya kusuasua mradi wa Liganga na Mchuchuma yatajwa
Mara baada ya Makamu wa Rais kununua jezi hiyo kwa Sh 5 milioni, kampuni mbalimbali zimeendelea kumuunga mkono kwa kutangaza kiasi cha fedha zinachopanga kutoa kwa ajili ya jezi hiyo.