Cairo, Misri. Beki wa Tanzania, Erasto Nyoni huenda akapona haraka majeraha yake na kucheza mechi dhidi ya Kenya utakaochezwa Alhamisi Juni 27, 2019.
Nyoni amekosa mechi ya kwanza dhidi ya Senegal kutokana na kusumbuliwa na majeruhi jambo lililomlazimisha kocha Emmanuel Amunike kumwanzisha David Mwantika pamoja na Kelvin Yondani
Akizungumza hali ya Nyoni, Daktari wa Stars, Richard Yomba alisema beki huyo alipata maumivu ya mguu wakati mechi ya kirafiki dhidi ya Zimbabwe.
Yomba alisema baada ya maumivu hayo walianza haraka kumpatia matibabu maalum mkongwe huyo, lakini akashindwa kuwa sawa muda mfupi kabla ya mchezo dhidi ya Senegal.
Alisema kwa sasa wanaendelea na uangalizi pamoja na matibabu zaidi ambapo hali yake inaendelea vyema na huenda akawa sehemu ya kikosi hicho katika mchezo ujao.
Aidha Yomba alisema ukiondoa Nyoni na Aggrey hakuna mchezaji mwingine majeruhi baada ya mchezo wa juzi na kila mmoja yuko sawa kuendelea na ratiba ya makocha.
Pia Soma
- Ndugai: Lishe duni ya wachezaji wetu imechangia Stars kufungwa
- Mbunge Chadema ‘ataja sababu’ kipigo cha Taifa Stars
- Mshambuliaji wa Taifa Stars ageuka kinyozi Misri