Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

MO Dewji ashangazwa na Cristiano Ronaldo ‘Dunia imejaa watu wenye macho ya husda’

8404 Mohammed Dewji 1k TZW

Mon, 28 May 2018 Chanzo: bongo5.com

/>

Mohammed Dewji

Sasa Mfanyabiashara maarufu nchini Tanzania na shabiki wa kutupwa wa klabu ya Simba, Mohamed Dewji ameibuka na mapya baada ya kuchukua picha iliyotrend kwenye mitandao ya kijamii ikimuonesha mshambuliaji wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo akimkata jicho Mo Salah kabla hata ya mchezo huo kuanza.



Mo Dewji ameweka picha hiyo na kuisindikiza kwa maneno “Tunaishi katika dunia ambayo imejaa watu wenye macho ya husda, fitna, unafki, na macho yaliyojaa wivu! Hakikisha unaenda na Mungu ili watu wenye macho mabaya wasiwe na nafasi ya kupenyeza ubaya katikati ya hatua zako za maisha (afya, elimu, ndoa, biashara)“.

Mo Salah mpaka sasa imeelezwa kuwa ana asilimia 80 ya kucheza kombe la dunia hii ni baada ya vipimo vya awali kufanyika usiku wa kuamkia leo.

Unadhani faulo aliyochezewa Mo Salah na mtukutu Sergio Ramos ni tukio la kimkakati yaani lilipangwa na Real Madrid au ni bahati mbaya?

_______________________________________________________________________________________________

Kwa sasa unaweza kupata habari zetu zote sehemu moja kwa kupitia App yetu ya Bongo5. Pakua sasa kupitia Play Store kwa kubonyeza link hii – https://bit.ly/2J2Argw

 

Loading...
Chanzo: bongo5.com