Kuelekea kilele cha Siku ya Vijana Duniani ambayo huadhimishwa kila ifikapo Tarehe 12 /8 kila mwaka, Wilaya ya Magharibi ‘A’ kupitia Baraza la Vijana imeandaa tamasha maalum la michezo katika kuelekea Siku hiyo ya Vijana Duniani
Katika mashindano hayo kutakua na michezo ya aina mbili kwa upande wa wanawake kunamchezo wa Nage na kwa wanaume kutakua na mchezo wa Mpira wa Miguu michezo yote hiyo itakuwa na timu 12 zinzoshiriki.
Timu ya Mwera ya Nage ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa chupa 29 huku Mfesenesini walitoka na chupa 12.
Na katika mchezo wa Mpira wa Miguu timu ya Welezo imeibuka na ushindi wa mabao 2 huku wenyeji wao Mwera walitoka bila ushindi wowote.
Tamasha hilo la michezo hiyo imefunguliwa na Abeid Juma Ali ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Magharib A.