Arusha.Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limesema wamelazimika kuongeza wachezaji wapya kwenye kikosi cha Timu ya Soka ya Vijana (Serengeti Boys) wakihofia kipimo cha MRI.
Katibu Mkuu wa TFF, Wilfred Kidau alisema timu hiyo sasa itakuwa na wachezaji 50.
Alisema wamelazimika kuongeza wachezaji wengine wakihofia baadhi ya waliokuwepo mwanzo kutokidhi vigezo watakapokwenda kwenye kipimo cha MRI.
"Tumeamua kuchukua tahadhari mapema, ili kuwachuja wale ambao wataonekana kuzidi umri isije kutokea kipindi cha mashindano," alisema Kidau na kufafanua.
"Tumefanya hivyo kwa kuwa hawa vijana, miaka imesogea, hivyo tunapaswa kujiridhisha mapema
Alisema vijana hao 50 watapimwa kipimo cha MRI mapema kabla ya kile watakachokuja kufanyiwa na CAF.