Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kioja Mademu Watatu Kuraruana Kilabuni Wakizozania DJ

D7ab62b351f29751 Kioja Mademu Watatu Kuraruana Kilabuni Wakizozania DJ

Thu, 25 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Burudani katika kilabu kimoja maarufu mtaani Umoja, Nairobi ilikatizwa kwa muda baada ya vidosho watatu kuanza kuraruana kwa kucha huku wakitwanganana wakizozania DJ.

Duru zinaarifu kuwa mabishano makali yalizuka pale ambapo mademu wawili kati yao walidai kwamba jamaa alikuwa mpenzi wao naye mwingine akashikilia ni mumewe mpendwa.

Kulingana na Taifa Leo, kama ilivyokuwa ada shughuli kilabuni humo zilikuwa zimeshika kasi huku waraibu wakijivinjari wakati warembo hao walipoingia nyakati tofauti tofauti.

Wakati warembo wakiingia, jamaa alikuwa kazini kwenye mitambo yake huku akiwaangushia waraibu vibao kwa ustadi.

Huku watu wakiwa wamezama kwenye muziki warembo hao watatu wasiojuana walimsongea mbele na bila hata kutoa tahadhari wakamshambulia DJ.

Mara fujo ikazuka baina yao huku kila mmoja akimwangalia mwenzake kwa macho makali.

“Mwache huyu ni chali yangu,” dada mmoja alidai huku akisema kuwa jamaa alikuwa amehepa baada ya kumpagawisha kwa penzi.

“Shughulikeni na wengine. Huyu simwachi ni mpenzi wangu,” wa pili naye alizuka na madai huku aiwasukuma wenzake.

“Sasa mkijadili ni wenu nami nitasemaje kwa kuwa ashanilipia mahari na nikazaa naye? Huyu ni mume wangu. Ondokeni hapa nyie,” kipusa wa tatu naye alipigania nafasi yake.

Penyenye zinasema kuwa fujo ilitanda kilabuni humo huku DJ akiburutwa na kutolewa nje akilishwa makofi mazito mazito.

Wateja waliokuwa wakijivijari walijaa hamaki kwa kukatiziwa sterehe yao.

Lakini pindi tu polisi walipowasili, kila mmoja wao alikuwa ni mguu niponye huku DJ naye pia akipata nafasi ya kutoroka.

Hata hivyo, haijulikana iwapo mademu hao walimsaka DJ huyo tena ili kumfunza adabu au la.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke