Mon, 26 Feb 2018
Chanzo: bongo5.com
Kikosi cha Simba kipo safarini kutoka mkoani Shinyanga kuelekea Mwanza ambapo usiku saa 1:00 kitaondoka jijini Mwanza kurejea jijini Dar es Salaam kwa usafiri wa ndege kupitia Shirika la ATCL.
Simba SC inatarajia kurejea Dar es Salaam huku ikiambulia sare ya magoli 2 – 2 katika mchezo wake wa mwisho dhidi ya Mwadui FC iliyocheza hapo jana.
Wakati kikosi hicho mpaka sasa kinaongoza katika msimamo wa ligi kuu kwa kuwa na jumla ya pointi 42 huku kikiwa kimecheza jumla ya michezo 18.
Chanzo: bongo5.com