Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kapombe: Tunaitaka Fainali Mapinduzi

KAPOMBE 1 Kapombe

Mon, 10 Jan 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

BEKI wa kulia wa Simba, Shomari Kapombe, amefunguka kuwa wanataka kushinda mchezo wao wa nusu fainali wa Kombe la Mapinduzi kwa kuwa wanataka kuibuka mabingwa wa kombe hilo.

Timu hizo mbili zinakutana leo Jumatatu katika mchezo wa Kombe la Mapinduzi hatua ya nusu fainali utakaopigwa Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Kapombe amesema kuwa; “Tunauchukulia huu mchezo kwa umuhimu sana maana tukikosea tutatoka. Namungo tunawajua maana tumetoka kucheza nao kwenye lligi muda sio mrefu.

“Kama wachezaji wa Simba tumejipanga kuweza kupambana kwa hali ya juu ili kuweza kuingia fainali na kuweza kuchukua kombe.”

Chanzo: www.tanzaniaweb.live