MATAJIRI wa Yanga walidhamiria timu yao itoke na ushindi leo baada ya kuwafanyia sapraizi wachezaji wao kwa kuwajaza mamilioni ya maana hata kabla ya kutinga uwanjani.
Yanga ambayo jana walikutana na mabosi wa klabu hiyo katika hafla ya kula chakula cha jioni.
Hafla hiyo iliyofanyika katika hotelli moja ya nyota nne matajiri hao bila wachezaji kutarajia wakajikuta wanakabidhiwa kiasi cha sh 15 milioni.
Fedha hizo zilikuwa kama mzuka kwa wachezaji hao kila mmoja alitamka atafia uwanjani na kupandisha morali kwa kiasi kikubwa.
"Viongozi wametupa hizo fedha kwakweli lilikuwa ni tukiola kutupa nguvu sana unajua klabu nyingi huwa hazipewi fedha taslimu tena kabla ya mechi,"alisema mmoja wa washambuliaji wa timu hiyo.