Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Juma Nyoso aachiwa ila mambo bado magumu

1925 Capture.PNGrrrrr.png TZW

Thu, 25 Jan 2018 Chanzo: bongo5.com

Swala la beki wa klabu ya Kagera Sugar, Juma Said Nyoso kumshambulia shabiki anaesadikika kuwa wa timu ya Simba, Shabani Hussein hadi kuzimia katika mchezo wao wa wiki hii uliyofanyika uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba bado halijakwisha licha ya Jeshi la Polisi kumuachia kwa dhamana mchezaji huyo.



Kupitia Mwanaspoti Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo, Issack Msengi amesema wamemwachia kwadhamana mchezaji Juma Nyoso wakati wakiendelea na upelelezi na ikibainika kuwa ana makosa atafikishwa mahakamani.



Shabiki anaesadikika kuwa wa timu ya Simba, Shabani Hussein ambaye anadaiwa kupigwa na mchezaji Juma Nyoso

“Kuhusu aliyejeruhiwa kwa sasa anaendelea vyema na kesho (leo) tunatarajia kupata ripoti ya kipimo cha Xray alichofanyiwa,” amesema Kamanda Msengi.

Kamanda Issack Msengi ameongeza kuwa wakimuachia Juma Nyoso baada ya kukamilisha taratibu za dhamana na wanaendelea kupeleleza kwa hatua zaidi huku akisema kama itabainika shabiki aliyepigwa alifanya kosa la jinai la kutukana hadharani nayeatafunguliwa kesi juu ya tukio hilo.



Beki huyo wa Kagera Sugar amejikuta akiingia mikononi mwa Jeshi la Polisi hapo juzi baada ya kutuhumiwa kumpiga shabiki na kumzimisha kitendo alichokifanya mara baada ya kumalizika kwa mchezo wao dhidi ya Simba SC uliyomalizika kwa kufungwa mabao 2-0 dhidi ya vinara hao wa ligi kuu soka Tanzania Bara.

 

Chanzo: bongo5.com