Meneja wa Manchester United, Jose Mourinho ametumia muda wake kumuandikia barua shabiki wa timu hiyo mzee mwenye umri wa miaka 94 badala ya kujiandaa dhidi ya Tottenham Hotspur mchezo utakao fanyika katika dimba la Wembley hapo kesho siku ya Jumatano.
Nakutakia maisha marefu shabiki, Fredrick Schofield na uweze kupata unafuu na kupona haraka dhidi ya ugonjwa huo wa kiarusi hii imekuja baada ya kumfuatilia kwa karibu.
“Sisi sote tumemevutiwa kwa kujitolea kwako kwa muda wote Manchester United,” ameyasema hayo Mourinho ndani ya barua yake.
“Nilitaka kukuandikia neno la shukurani kwa sapoti yako na kujitolea kwako ndani ya klabu hii.”
Mourinho amesaini barua hiyo aliyomuambia Schofield kwamba yeye mwenyewe, wachezaji na wafanyakazi wote wanamfikiria hali ambayo familia yam zee huyo ilishikwa na bumbuwazi kwa kuipata barua hiyo iliyoelekezwa kwenda kwa kikongwe huyo.
My grandad was made up with it, I'm a City fan however credit where credits due. When I contacted them I didn't expect this, United exceeded my expectations here. Football passion in our city is amazing, divides us but can unify us when needed. pic.twitter.com/QKuonZHecC
— Kieran Schofield (@Kieran18m) January 27, 2018