Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

James Maddison kufanyiwa vipimo kukamilisha usajili Leicester

9486 Skysports James Maddison Norwich Championship 4196215 TZWeb

Mon, 18 Jun 2018 Chanzo: bongo5.com

Klabu ya Norwich City FC imeridhia ofa ya pauni milioni 20 kutoka kwa Leicester ili kumuachia kiungo wake mshambuliaji, James Maddison mwenye umri wa miaka 21 kujiunga na Mbweha hao wa Uingereza.



Maddison anayekipiga kwenye timu ya vijana ya Uingereza anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya wiki hii tayari kujiunga na Leicester baada ya kuhuhusishwa kwa muda mrefu kuhamia Southampton.

Kinda huyo wa Norwich amefanikiwa kufunga jumla ya mabao 15 kwenye michezo yake 49 aliyocheza msimu uliyopita huku klabu hiyo ikitarajia kuvuta mkwanja huo mrefu ukilinganisha na wachezaji wake wengine waliyopata kuwauza.

Loading...
Chanzo: bongo5.com