Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Jack van Poortvliet: kurejea uwanjani baada ya kukaa nje miezi nane

Jack Van Poortvliet: Kurejea Uwanjani Baada Ya Kukaa Nje Miezi Nane Jack van Poortvliet: kurejea uwanjani baada ya kukaa nje miezi nane

Thu, 21 Mar 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Muingereza Jack van Poortvliet anatarajiwa kurejea baada ya kukaa nje ya uwanja kwa muda wa miezi minane baada ya kuwekwa benchi na Leicester katika mchezo wa Ijumaa dhidi ya Gloucester.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 aliondolewa kwenye michuano ya Kombe la Dunia mwaka jana nchini Ufaransa kutokana na jeraha la kifundo cha mguu.

Itakuwa mechi ya kwanza kwa Van Poortvliet chini ya bosi wa Tigers Dan McKellar.

"Sote tumefurahi sana kumuona Jack akiwa sawa, mwenye afya njema na amevaa jezi ya Tigers," McKellar alisema.

Van Poortvliet mzaliwa wa Norwich, ambaye alipitia akademi ya Tigers, alicheza mara ya mwisho mnamo Agosti 2023 alipopata jeraha dhidi ya Wales katika kujiandaa kwa Kombe la Dunia.

Hapo awali alizungumza juu ya "kuhuzunishwa" na kukosa mashindano hayo, ambapo England iliendelea na kumaliza katika nafasi ya tatu.

Kurejea kwa mchezaji huyo akiwa sawa kimwili kunalingana na kurejea kwa michuano ya Ligi Kuu baada ya kusimama kwa miezi miwili ili kwendana na Mataifa Sita.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live