Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Iniesta atangaza rasmi kuondoka Barcelona, machozi yamwagika hadharani

7159 4B9C97C000000578 5664537 Image A 38 1524829962550 TZW

Sun, 29 Apr 2018 Chanzo: bongo5.com

Kiungo mkongwe wa Barcelona na timu ya taifa ya Hispania, Andres Iniesta ametangaza ataondoka kwenye klabu hiyo mara baada ya msimu huu kumalizika.



Iniesta (33) amedumu ndani ya Barcelona tangu mwaka 1996 alipojiunga na timu ya vijana, tayari mpaka sasa ameshachukua vikombe 31 akiwa na timu hiyo.

Mchezaji huyo alianza kuichezea timu ya wakubwa ya Barca 2002 na amecheza mechi 669 wakati kipindi hicho akiwa na umri wa miaka 18.

Iniesta ametangaza maamuzi hayo huku akitokwa na machozi leo katika mkutano wake ambao ulihudhuriwa na mbele ya mkewe na watoto wake, baadhi ya wachezaji wenzake wa Barca na rais wa timu hiyo Josep Maria Bartomeu.



Kiungo huyo anatarajiwa kujiunga na Chongqing Dangdai inayoshiriki ligi kuu ya China. Hata hivyo klabu ya Manchester City imeonekana kumuhitaji mchezaji huyo.

Chanzo: bongo5.com