Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Hivi ndivyo matokeo ya mechi za leo yalivyo badili msimamo mzima wa VPL

3549 Azam.png TZW

Mon, 26 Feb 2018 Chanzo: bongo5.com

Ligi kuu soka Tanzania Bara imeendelea tena hii leo kwa michezo miwili kupigwa katika viwanja tofauti.



Kikosi cha Mtibwa Sugar kimekubali kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Ruvu Shooting katika dimba la Manungu wakati Tanzania Prisons ikiibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mwadui FC katika uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

Kwa matokeo hayo Tanzania Prisons imepanda hadi nafasi ya tano ikiishusha Mtibwa Sugar, huku Ruvu Shooting ‘Wazee wa kupapasa’ wakizidi kuchanja mbunga hadi namba saba.

Michezo iliyosalia kukamilisha raundi hii ni vinara wa ligi hiyo timu ya Simba dhidi ya Mbao wakati Ndanda ikiwa na kibarua kizito cha kuivaa Yanga SC.

Chanzo: bongo5.com