Harry Kane atimiza idadi ya magoli 100 katika Ligi Kuu ya uingereza baada ya kuweza kushinda penati ya pili katika mechi ya Tottenham dhidi ya Liverpool siku ya Jumapili jana.
Mshambuliaji huyo wa Uingereza amekuwa mchezaji wa pili kufikia hatua kubwa zaidi akiwa nyuma ya Alan Shearer,baada ya kusawazisha goli dakika za mwisho huko Anfield na kufanya watoke sare ya 2-2 na Liverpool.
Kane, alipatwa na ujasiri wa kugonga nyuma ya wavu baada ya kukosa penati ya kwanza ambayo ingeweza kuwafanya Spurs kupata uongozi wa 2-1.
Mbali na hayo Kane alisema kwamba alikuwa tamaa ya kufunga mara baada tu ya kipa wa Liverpool Loris Karius kuokoa penati na pale ambapo Mohamed Salah alipofunga goli lake la pili katika mchezo huo na kuwafanya Liverpool kuwa mbele katika dakika ya 91.
Kane, ambaye alifunga bao lake la 22 la msimu huu na pia la 100 katika mechi 141 alizocheza kwenye Ligi kuu ya Uingereza , aliiambia Sky Sports Main kuwa “Nilikuwa nikiomba.
“Hutarajii hasa wakati wa dakika za mwishoni lakini nina shukuru sana baada ya kupata nafasi ya pili na nina furahi sana kufikisha idadi ya magoli 100 katika Ligi Kuu na nina furaha sana ya kuwa miongoni mwa wachezaji kufikisha magoli 100.”
Kampuni ya Nike wamemtengenezea kiatu cha kipekee kiitwacho Nike Hypervenom 3 HK ambacho atakivaa Kane katika mechi yake ijayo. Viatu 100 ndiyo idadi ya viatu hivyo vilivyo tegenezwa na vina rangi nyeupe na rangi ya bluu na zitapatikana madukani hapo baadaye.
Kane amekuwa mchezaji wa 26 kufikisha idadi ya magoli 100 katika Ligi Kuu ya Uingereza akiwa mbele ya Sergio Aguero katika orodha ya hiyo.
Na Raheem Rajuu