Lewis Hamilton amerejea kwenye timu yake ya Mercedes wiki hii kujiandaa na msimu mpya wa langalanga ambapo hapo awali majaaliwa ya ushiriki wake ulikuwa ukitiliwa shaka kutokana changamoto zilizojitokeza kwenye mashindano ya kumpata bingwa kwa mwaka 2021(Abu Dhabi Grand Prix 2021).
Lewis Hamilton amerejea kwenye timu yake ya Mercedes wiki hii kujiandaa na msimu mpya wa langalanga ambapo hapo awali majaaliwa ya ushiriki wake ulikuwa ukitiliwa shaka kutokana changamoto zilizojitokeza kwenye mashindano ya kumpata bingwa kwa mwaka 2021(Abu Dhabi Grand Prix 2021). Hamilton 37 ambaye ametwaa taji la langalanga mara saba, siku ya Jumatatu na Jumanne alimaliza majukumu yake na kujiandaa na mbio za msimu huu huku baadhi ya vipande vya video akiviweka kwenye mtandao yake ya kijamii.