NI Mwijaku ambae leo Agosti 5, 2021 amezungumza na Vyombo vya Habari kuhusu kauli za Haji Manara alizozitoka Agosti 4, 2021 akishtumu Uongozi wa Simba SC.
“Mimi nimesikitishwa sana na Haji jana kuanza kumkebei Mo Dewji muwekezashaji alieweka Simba Sport Club Bilioni 21 kitendo cha kumkebei na kusema amekopa mimi nimwambie Haji anitafutie Bilionea yoyote hapa Duniani ambae hajawahi kukopa aniambie amefanikiwa vipi kila unaemuona Bilionea popote pale basi lazima awe amekopa”- Mwijaku
.
“Swala la kumkebei Mo Dewji naomba kwanza afute kauli kuwekeza katika Simba SC akuhitaji hela atoe mfukoni ama atoe Benki unaposema Mo Dewji amekopa basi amekopa kutokana na kazi zake”- Mwijaku
.;
“Ametoa historia ya watu waliondoka Simba SC ametaja zaid ya watu 15 akidai kuwa wameshtumiwa wanahujumu timu mimi nimwambie tu kitu kimoja Haji katika maisha hauwezi kukaa sehemu miaka yote”-Mwijaku