Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Europa League: Griezmann awabana Arsenal nyumbani, Marseille wapeta

7127 4B96474500000578 5661827 Lacazette Battles For Possession With Griezmann Who Earlier Miss A 136 TZW

Sat, 28 Apr 2018 Chanzo: bongo5.com

Usiku wa jana michezo ya nusu fainali ya kombe la Europa League imechezwa ambapo Arsenal wakiwa kwenye uwanja wa Emirates wametoka sare ya kufungana bao 1-1 na Atletico Madrid ya Hispania.



Arsenal ndio walikuwa wakwanza kufunga goli lao kupitia kwa acazette dakika ya 61 wakati bao la Atletico lilifungwa na Antoine Griezmann dakika ya 82.

Katika mchezo huo Atletico walilazimika kucheza wachezaji 10 uwanjani baada ya beki wao Sime Vrsaljko kuonyeshwa kadi nyekundu katiaka dakika ya 10 ya kipindi cha kwanza.

Wakati huo huo kwenye nusu fainali nyingine, Olympique de Marseille ya Ufaransa walikuwa nyumbani walifanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya RB Salzburg ya Austria.



Mabao ya Marseille yalifungwa na Thauvin (15) na Clinton N’jie (63).

Chanzo: bongo5.com