Mon, 26 Mar 2018
Chanzo: bongo5.com
Kiungo wa Misri Mohamed Elneny amesaini mkataba mpya wa kuendelea kuichezea Arsenal kwa kipindi kirefu.
Elneny alisajiliwa akitokea Basle mwezi January maka 2016 na ameshaichezea Arsenal michezo 65.
Baada ya kusaini mkataba huo, Elneny ameandika kwenye mitandao yake ya kijamii ujumbe unaosomeka, “Officially we will be together for a longer time, in order to reach what we started, and to put arsenal in it’s deserved spot In Europe and the whole world.”
Hata hivyo bado haijafahamika ni mkataba wa muda gani ambao ameongeza kuiheza timu hiyo.
Chanzo: bongo5.com