Katibu Mkuu wa Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo Dkt. Abbasi leo ameutangazia Umma wa Watanzania na wapenda Michezo kwamba leo asubuhi wamekabidhiwa rasmi eneo la Ekari 12 Tanganyika Packers kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Arena kubwa na ya kwanza nchini kwa ajili ya Michezo na Sanaa.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo Dkt. Abbasi leo ameutangazia Umma wa Watanzania na wapenda Michezo kwamba leo asubuhi wamekabidhiwa rasmi eneo la Ekari 12 Tanganyika Packers kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Arena kubwa na ya kwanza nchini kwa ajili ya Michezo na Sanaa. Dkt. Abbasi ambaye ameiita hii kama zawadi ya Valentine’s kwa Watanzania ikiwa leo ni siku yake ya kuzaliwa, amesema mwezi ujao Mkandarasi atakabidhiwa site kwa ajili ya kuanza hatua za ujenzi.