Dar es Salaam. Kocha w Simba, Mbelgiji Patrick Aussems amebadilisha nguo mara mbili wakati wa mchezo wao na Yanga leo Jumapili ya Septemba 30.
Aussems ambaye aliingia uwanjani kwa mara ya kwanza wakati timu yake ikipasha moto misuli akiwa amevaa tisheti nyeusi.
Katika mazoezi hayo yeye hakusimamia alisimama pembeni akichungulia, yaliongozwa na wasimamizi wake akiwemo, Masoud Djuma.
Lakini, airudi tena uwanjani kwa ajili ya kuongoza mechi.
hapo ndipo alikuwa amevalia shati nyeupe badala ya ile tisheti nyeusi na alidumu nayo kwa dakika 90, za mchezo.
Hali hii si kawaida kwa kocha kubadili nguo mara mbili wakati wa mchezo, kawaida huwa ni moja.
Kitendo hicho hutokea kwa wachezaji ambao huingia na aina moja ya jezi kwa ajili ya kupasha misuli na baadaye hubadilisha zile za kuchezea mechi.