Rapa maarufu wa Canada, mwimbaji na mtunzi wa nyimbo Drake ameshinda dola milioni 2.7 (Tsh bilioni 6.28 ) baada ya Bondia Israel Adesanya wa Nigeria kumbwaga Alex Pereira raia wa Brazil kwenye UFC 287 na kutetea tena taji lake la uzito wa kati.
Adesanya alishinda tena taji hilo kwa KO katika raundi ya pili miezi mitano tu baada ya kushindwa na Pereira, ambaye hapo awali alimshinda mara mbili katika mchezo wa ndondi.
Drake alipoteza dola milioni 1.6 baada ya kumwekea dau Adesanya kushinda katika pambano hilo lakini amepindua meza kibabe baada ya kumwamini tena Adesanya katika mechi ya marudiano na Pereira Jana Jumamosi usiku huko Miami.
Drake aliweka dau la $500,000 kwa Adesanya kushinda na kujishindia $885,000 lakini pia aliweka dau la $400,000 ili ashinde kwa KO na kujikusanyia dola milioni 1.8 ambapo jumla ameshinda takribani dola milioni 2.7