Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Donald Kipkorir akerwa na mazoea ya matajiri kuomba misaada ya mazishi

A5b7610ae2fad507 Donald Kipkorir akerwa na mazoea ya matajiri kuomba misaada ya mazishi

Thu, 20 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Wakili Donald Kipkorir ameduwazwa na familia tajiri ambazo zimekuwa na mazoea ya kuomba misaada ya kifedha ili kugharamia mazishi ya jamaa zao wanapofariki dunia

- Kipkori r ameshangaa ni nani atawazika maskini iwapo matajiri hawawezi kujitegemea

- Jane Wanjiru Rika ambaye alikuwa mke wa Kaptein Josephat Rika na dadake marehemu mama Lucy Kibaki aliaga dunia Jumamosi, Mei 15 na familia yake inaomba msaada wa mazishi

- Ezekiel Mutua aliunga mkono kauli ya Kipkorir akisema ina uzito sana na watu tajiri wanapaswa kuacha mwenendo huu

Wakili tajika Donald Kipkorir amekashifu vikali familia tajiri ambazo zimekuwa zikiitisha misaada ya kifedha kila zinapopatwa na msiba.

Kipkorir alishangaa na baadhi ya familia zenye mazoea hayo na kwa kauli yake familia maskini ndio zafaa kuomba msaada.

" Familia tajiri zikianza kuomba msaada wa kifedha kugharamia mazishi ya mpendwa wao, ni nani atakayemzika maskini?, kwani ni kiwango kipi kinahitajika kumzika mtu, mbona watoto wake, wajukuu, binamu na wajomba wasiungane na wanunue jeneza, wachimbe kaburi na wampe mpendwa wao heshima za mwisho anazostahili?," Kipkorir aliandika Twitter.

Kulingana na wakili huyo, serikali inapaswa kupiga marufuku michango ya mazishi kabisa.

Madai ya Kipkorir yalionekana kuilenga familia ya Rais Mstaafu Mwai Kibaki kufuatia kifo cha ya shemeji yake Jane Wanjiru Rika maarufu Nee Kagai.

Wanjiru alikuwa mke wa kaptein Josephat Rika na ni dadake marehemu Mama Lucy Kibaki, alifariki dunia Jumamosi, Mei 15 baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Kupitia kwenye tangazo katika gazeti la Daily Nation, familia ya mwendazake ilikuwa imeomba msaada wa kifedha kugharamia mazishi yake.

" Ni huzuni mkubwa lakini kwa mapenzi ya Mungu, tunakitangaza kifo cha mama, nyanya, dada na rafiki Jane Wanjiru Rika ( Nee Kagai) kilichotokea Jumamosi, Mei 15, 202i," Sehemu ya tangazo hilo ilisoma.

" Tungependa kumpa heshima zake za mwisho mpendwa wetu kwa njia ya kipekee, tungependa wahisani watume mchango wao kwenye nambari ya Pay- bill 8022025 na akaunti ikiwa jina la anayetuma," Sehemu nyingine ya tangazo hilo ilisoma.

Mwili wa marehemu utaondolewa katika hifadhi ya wafu ya hospitali ya Outspan mjini Nyeri siku ya Jumanne, Mei 25 na hafla ya mazishi kufanyika siku hiyo hiyo nyumbani kwake kijijini Naromoru.

Aidha, kauli ya Kipkori iliungwa mkono na mwenyekiti wa bodi ya kudhibiti filamu nchini, Ezekiel Mutua ambaye pia aliwashauri matajiri dhidi ya kuitisha misaada akidai sio maadili mema.

Mutua alisema madai yaliotolewa na Kipkorir yana uzito zaidi na serikali inapaswa kuyachunguza na kupata suluhu.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zidi kutoka TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke