Thu, 2 Aug 2018
Chanzo: mwananchi.co.tz
Kartepe. Kiungo mpya wa Simba, Hassan Dilunga ni kama tayari ameingia kwenye kikosi cha kwanza cha kocha Mbelgiji Patrick Ausemms.
Hii ni kutokana na namna anavyowatumia katika uchezaji.
Dilunga ni mchezaji mpya wa Simba amesajiliwa kutoka Mtibwa Sugar ni kama anamshawishi kocha huyo anayesisitiza soka la kuchezea mpira na pasi.
Amekuwa akimtumia zaidi katika kila kikosi cha timu anayoijaribu kimfumo.
Hata hivyo, Ausemms amesema bado anaangalia wachezaji ili kupata wa kikosi cha kwanza.
Chanzo: mwananchi.co.tz