UJIO wa kipa Djigui Diarra umekuwa mwiba kwa Faruk Shikhalo baada ya uongozi wa timu hiyo kuamua kuachana naye baada ya kumpa barua ya kumuacha.
Diarra amepishana na makipa wote wawili mzawa na mgeni ambao wameipambania timu hiyo kumaliza nafasi ya pili inayowafanya waweze kushiriki Ligi ya Mabingwa msimu huu.
Kwa mujibu wa chanzo cha ndani Yanga kimesema sasa watakuwa na Diarra aliyechukua nafasi ya Faruk na Erick Johora ambaye ni Mtanzania aliyekuwa anakipiga Burundi.
Shikalo ameachana na timu hiyo baada ya mkataba wake kumalizika na uongozi kufikia uamuzi wa kuto kumuongeza mkataba mwingine.