Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Daniel Sturridge atimka Liverpool

2217 DUvPR4TWkAIdrrF TZW

Tue, 30 Jan 2018 Chanzo: bongo5.com

Mshambuliaji wa klabu ya soka ya Liverpool, Daniel Sturridge amejiunga kwa mkopo na timu ya West Brom mpaka mwisho wa msimu huu.



Sturridge amejiunga na timu hiyo baada ya kuonekana kukosa namba katika kikosi cha Liverpool tangu alipowasili kocha Jürgen Klopp mwaka 2015.



Baada ya kufanikiwa kukamilisha uhamisho wake huo wa mkopo na kukabidhiwa jezi yake yenye namba 15 ambayo amezoea kuivaa, mchezaji huyo amesema, “Nilifahamu hii itakuwa klabu sahihi kwangu. Nina marafiki hapa nilicheza nao kabla, meneja alizungumza vizuri na kuna changamoto ya timu na mtindo wa kucheza.”

Awali mchezaji huyo alikuwa anawaniwa na timu kadhaa ikiwemo Newcastle United.



Chanzo: bongo5.com