Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Coastal yakana kumtimua Mgunda

Coast ED.jpeg Coastal yakana kumtimua Mgunda

Tue, 4 May 2021 Chanzo: ippmedia.com

Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Rashid Mgweno, ameeleza kushangazwa na taarifa hizo na kuongeza wao kama viongozi hawajawaza ama kufikiria jambo hilo kutokana na kocha huyo alivyo ndani ya klabu hiyo.

"Tunazikanusha, hazina ukweli wowote, ni taarifa za uongo. Hatujui zimetokea wapi, lakini tunaendelea kuzifuatilia ili tuchukue hatua kwa sababu zimezua taharuki kwa wanachama na mashabiki wetu, sisi viongozi hata na mwenyewe pia," alisema katibu huyo.

Alisema kuwa Mgunda kwenye klabu ya Coastal si kocha tu kama watu wanavyoona kwa nje, lakini amekuwa zaidi ya kocha, kwani kuna vitu amekuwa akiisaidia klabu hiyo kwenye kuisogeza mbele kupata mafanikio.

"Sisi hatumchukulii kama ni kocha, bali ni kiongozi pia, wakati mwingine anafanya majukumu ambayo si ya kiualimu, bali kama kiongozi ambavyo watu wengi hawaelewi ndiyo maana sisi viongozi hatujawahi hata kuwaza kumfukuza, kwa sababu tunajua na tumfahamu," alisema.

Chanzo: ippmedia.com