Dar es Salaam.Mshambuliaji wa Taifa Stars, Shabani Chilunda alishindwa kumaliza mazoezi ya timu hiyo yakiyofanyika leo Jumatatu asubuhi baada ya kuumia kifundo cha mguu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Chilunda aliumia katika mazoezi hayo kifundo cha chini cha mguu wa kulia na kushindwa kumaliza mazoezi hayo na wenzake jambo ambalo madaktari wa timu walilazimika kumfunga bandeji mguuni iliyomsaidia kutembea mpaka kwenye gari la wachezaji.
Katika hatua nyingine Chilunda pamoja na klabu yake ya Azam wamefikia makubaliano na klabu yake ya kuachana na CD Tenerife ya Hispania.
Chilunda msimu huu amecheza mechi tatu katika klabu yake ya CD Tenerife kabla ya kupelekwa kwa mkopo CD Izarra.
Uongozi wa CD Tenerife ukichukua nafasi hiyo kumtakia kila la kheri huko aendapo na msimu ujao hata kuwa katika orodha ya wachezaji wa kikosi hiko.
Chilunda alisema wamefikia makubakiano na klabu yake ya CD Tenerife ya kuachana kwa amani na anaweza kwenda kujiunga na timu yoyote.
Pia Soma
- Makonda atimiza ahadi Simba, amkabidha Manula Sh10mil
- Kitambi cha Chioma gumzo Nigeria
- Samatta apewa mtaa Dar es Salaam
"Timu zipo si moja ila ambayo nitakubaliana nayo nitajiunga nayo na wao ndio watakuwa na mamlaka ya kuliweka wazi jambo hili lakini kwa sasa siwezi kueleza nitakwenda timu gani.
"Suala na kurudi Azam kwa kipindi hiki ni hapana nitakuwa tena nje ya Tanzania," alisema Chilunda.