Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Chama asimamisha kwa muda mkutano wa Simba

Clatous Chama Of Simba Sc 1ol92pcj2lifp1ozpnrt7266aw Chama asimamisha kwa muda mkutano wa Simba

Sun, 21 Nov 2021 Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz

Kiungo wa Berkane ya Morocco, Cletous Chama amesimamisha kwa muda hotuba ya Kaimu Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya Simba, Salim Abdallah 'Try Again' kwenye mkutano mkuu wa klabu hiyo.

Wanachama walilipuka kwa furaha wakati Try Again alipowaeleza kumsajili mchezaji yoyote wanayemtaka baada ya mwekezaji wa klabu hiyo, Mo Dewji kumhakikishia mzigo upo.

Kaimu Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya Simba, Salim Abdallah 'Try Again' alipokuwa akizungumza na wanachama wa klabu hiyo leo katika mkutano mkuu wa Simba.

"Tutamleta yeyote, sijui awe Chama au nani, amesema Try Again na kushangiliwa kwa nguvu na wanachama wengine wakisimama na kutoa maneno ya kujisifu, hali iliyosababisha Try Again kusimama kwa sekunde kadhaa kusubiri wanachama wanalize kushangilia.

Kabla ya kumtaja Chama aliyeuzwa na klabu hiyo, Try Again alisema bodi ya Wakurugenzi imempa urais wa heshima Mo Dewji kwenye klabu hiyo kutokana na namna aluvyojitoa ndani ya klabu.

"Amenihakikishia pesa ipo, tutasajili yeyote tunayemtaka," amesisitiza Try Again kwenye mkutano huo unaoendelea jijini Da es Salaam.

Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz