Timu ya Chuoni FC inayoshiriki Ligi Kuu Soka Zanzibar Leo Agosti 31, 2020 imemtambulisha kocha wao wa magolikipa Yussuf Ali “Sunji” kocha huyo atashirikiana na kocha Mkuu Ali Bakar (Mgazija) mwenye Leseni B ya CAF aliyefunga mkataba wa miaka 2 kuitumikia timu hiyo.
Mngazija amechukuwa nafasi ya Ramadhani Madundo ambae alioondoka klabuni hapo.
Kocha huyo ambae alishawahi kuifundisha timu hiyo kwa mafanikio makubwa ambapo mwaka 2014 aliisaidia kucheza Mashindano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika ambapo Chuoni ilitolewa hatua ya awali na timu ya How Mine Fc ya Zimbabwe.
Kwa habari za michezo tembelea www.dimbani.co.tz